
Zanzibar ni moja kati ya maeneo mengi nchini Tanzania ambayo yanasifika kuwa na wachezaji nyota ambao hufunzwa soka tangu wakiwa vijana wadogo hadi wanapokuwa wakubwa.
Mifano ipi mingi, akiwemo mwanasoka wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania Abdi Kassim Babi, Nyota anayeitumikia Azam kwasasa Feisal Salum, Mudathir Yahya, Maabadi Maulid Maabad anayeitumikia Coastal Union na wengine wengi.
Licha ya sifa zote hizo kutoka kwenye kisiwa cha karafuu, lakini bado Ligi yao imekuwa haina mvuto mkubwa kama zilivyo Ligi zingine ikiwemo Ligi kuu kandanda Tanzania Bara.
Ally Mohamed ni Afisa habari wa klabu ya Mlandege ambayo imekuwa na mafanikio makubwa kwenye mashindano ya Mapinduzi Cup kwa misimi hii miwili ikifika fainali [2023 – Bingwa, 2024 – Fainali vs Simba], yeye ameeleza sababu kadhaa zinazopelekea Ligi ya Zanzibar kukosa mvuto.
- Timu hazina maandalizi ya kutosha.
Tmu nyingi kutoka visiwani Zanzibar hazina utaratibu wa kuweka kambi, mara nyingi huweka kambi siku ya mchezo husika.
“Ukiangalia kwa Bara timu zinaweka kambi kwa muda mrefu lakini huku kwetu Zanzibar timu zinaweka kambi siku ya mchezo”.
“Wanaweza kukutana saa nne asubuhi hadi muda wa mchezo na baada ya hapo kila mmoja anasambaa anaendelea na kazi zake”, alisema Ally Mohamed.
• Miundo mbinu
Kabla ya ujenzi wa uwanja wa New Amaan Complex ni viwanja viwili tu ambavyo vinatumika kwaajili ya michezo yote ya Ligi kuu Zanzibar kitu kinachopoteza ladha ya mpira.
“Kabla ya uwanja wa New Amaan tulikuwa na viwanja viwili, uwanja wa finya [Pemba] na Mao [Unguja], kiuhalisia ni uwanja ambao unatumika kwenye Ligi lakini ukifuata mahitaji ya uwanja unaona vina mapungufu makubwa”. Alisema Ally.
- Umbali
Ally Mohamed anasema mara nyingi timu inasafiri kwa takribani saa kumi [10] na wanakuwa na muda mchache wa kupumzika hivyo ushindani unakuwa mdogo.
“Ukicheza mechi mbili [2] kwa Unguja, utacheza na klabu ambazo ziko Unguja, ukicheza ugenini kwa klabu ambazo ziko unguja, utacheza hapo hapo uwanja wa Mau”.
“Ukicheza na klabu za Pemba lazima usafiri, na ni umbali mrefu sana na usafiri tunaoutumia ni wa majini, ni takribani masaa nane unakaa kwenye maji kuifuata timu”.
“Tunachukua saa takribani 10, kwenye maji nane na barabarani mbili kuifuata timu, ukifika hapo pengine una siku moja tu, kwa kiasi fulani ufanisi unakosekana”, Ally aliongeza.
- Uchumi
Timu nyingi hazina wadhamini wao binafsi kitu ambacho kina wafanya watumie pesa nyingi sana na wakati mwingine wanashindwa kutimiza baadhi ya vitu mhimu ikiwemo usajili wa nyota wakubwa kama ilivyo kwa Ligi zingine.
“Mdhamini sio kila kitu, klabu katika swala la uendeshaji, fedha wanazozipata kutoka kwa hawa wadhamini zinaweza kumalizika kabla hata nusu ya msimu haijakamilika”, aliongeza Ally.
Mashabiki wa soka visiwani Zanzibar bado hawaamini katika kile kinachotolewa na klabu zao za nyumbani na asilimia kubwa ya watu hapa ni mashabiki wa timu za Tanzania Bara [Simba na Yanga].
“Hapa kwetu vipaji vipo lakini Ligi yetu haichezwi kama ilivyo kwa Tanzania Bara, na hata zingeingia timu za hapa kwetu fainali ya mapinduzi ungeona mashabiki wachache uwanjani, huku kwetu hakuna ushindani” Alisema shabiki mmoja.
Ligi yoyote ili iweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa lazima kuwe na uwekezaji mkubwa kutoka kwa wadhamini pamoja na klabu zenyewe, kwa maeneo ya Zanzibar asilimia kubwa ya watu wanapenda sana kuangalia mpira.

Makala Nyingine
-
Makala Nyingine
/ 1 year agoUWANJA WENYE HISTORIA YA PELE NA MARADONA KUFUNGUA WORLD CUP.
Shirikisho la soka Duniani FIFA limetangaza rasmi tarehe ya ufunguzi wa fainali za kombe...
By Lamarcedro -
Tetesi za usajili
/ 1 year agoCHAMA KUONDOKA SIMBA JUNE 2024.
Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba raia wa Zambia Clatous Chotta Chama mkataba wake...
By Lamarcedro -
Makala Nyingine
/ 12 months agoZEROBRAINER0 : NA DUNIA YAKE YA MITANDAO YA KIJAMII
Kwenye Vitabu vya Historia ya wachezaji nguli kweli kweli waliowahi Kutamba na Mtibwa Sugar...
-
-
CAF Champions League
/ 12 months agoNI ESPERANCE V AL AHLY CAF CHAMPIONS LEAGUE
Esperance Watakuwa wenyeji wa Al Ahly kwenye mchezo wa kwanza wa Fainali ya Ligi...
-
Azam Sports Federation
/ 1 year agoHII HAPA RATIBA CBFC ROBO FAINALI NA NUSU FAINALI
Droo ya Kombe la CBFC(CRDB BANK FEDERATION CUP) 2024 Hatua ya Robo Fainali imechezeshwa...