Connect with us

CAF Champions League

MECHI TISA [9] CAF CL KWA YANGA BILA USHINDI.

Klabu ya Yanga haijawahi kupata ushindi wowote kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa Barani Afrika tangu Ligi hii ianzishwe.

Yanga imecheza jumla ya mechi tisa [9] imetoa sare michezo minne [4] na imepoteza michezo mitano [5], imekusanya alama nne [4] pekee.

Leo Yanga inashuka dimbani katika uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Medeama katika mwendelezo wa Ligi ya mabingwa Barani Afrika hatua ya makundi ukiwa ni mchezo wa nne [4] msimu huu.

Yanga msimu huu kwenye Ligi ya mabingwa Afrika hatua ya makundi imefunga magoli mawili [2], imeruhusu magoli matano [5], imekusanya alama mbili [2].

Makala Nyingine

More in CAF Champions League