FIFA World Cup

SENEGAL YAITAKA FIFA KUIONDOA UFARANSA WORLD CUP.

Published on

Timu ya taifa ya Senegal imeliandikia barua Shirikisho la soka Duniani FIFA kutekeleza sheria na kuiondosha timu ya Taifa ya Ufaransa kwenye fainali za kombe la Dunia chini ya miaka 17 zinazoendelea hivi sasa nchini Indonesia kwa kumtumia nyota Yanis Ali Issoufou Abdoulkadre.

Kwa mujibu wa barua hiyo inaeleza kuwa nyota huyo aliitumikia timu ya Taifa Niger wakati wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali hizo na baadae akaibukia kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Ufaransa kwenye fainali hizo zinazoendelea nchini Indonesia.

Senegal na Ufaransa zilikutana hatua ya 16 bora na Ufaransa ikasonga mbele hatua ya robo fainali baada ya kuiondosha Senegal kwa mikwaju ya Penati 5-3 kufuatia suluhu ya 0-0 baada ya dakika tisini kumalizika. Kabla ya mchezo huo Senegal iliwasilisha malalamiko ya mchezaji huyo na mwisho wa siku Ufaransa hawakumtumia nyota huyo kwenye mchezo huo.

Kwasasa fainali hizo zimefika hatua ya robo fainali, Africa hadi hivi sasa imebakiza timu mbili pekee, Mali na Morocco ambazo zitakutana hatua ya robo fainali, timu zingine zilizofuzu hatua ya robo fainali ni Ufaransa, Uzbekistan, Brazil, Argentina, Hispania na Ujerumani.

MECHI ZIJAZO

NOVEMBER 24,2023

11:30 SPAIN vs GERMANY

UWANJA: Jakarta International

NOVEMBER 24, 2023

15:00 Brazil vs Argentina

UWANJA: Jakarta International

NOVEMBER 25, 2023

11:30 FRANCE vs UZBEKISTAN

UWANJA: Manahan Stadium [Surakarta]

NOVEMBER 25

15:00 MALI vs MOROCCO

UWANJA: Manahan Stadium [Surakarta].

Popular Posts

Exit mobile version