Mwamuzi wa soka nchini Ghana Kenney Padi amesema tangu alipoipatia penalty klabu ya Heart Of Oak katika mchezo wa Ligi dhidi ya Asante Kotoko sehemu zake za siri hazifanyi kazi.
Mchezo huo ulipigwa April 10, 2022 ambapo Heart Of Oak walishinda goli 1-0 lililofungwa kwa mkwaju wa penalty na Frank Mbella Etouga.
Sehemu zangu za siri hazifanyi kazi tangu niipatie mkwaju wa Penalty Heart of Oak.
Muda mwingine napata ndoto za kutisha siwezi kulala.
Kenney Padi, Mwamuzi wa soka Ghana.