AFCON

SHALULILE KUITIKISA AFRIKA LEO MBELE YA TUNISIA.

Published on

Match : Tunisia vs Namibia .
Uwanja : Amadou Gon Coulibaly.
Mji : Korhogo, Ivory Coast.

Timu ya Taifa ya Tunisia itashuka dimbani kwenye mchezo wake wa kwanza wa fainali za mataifa ya Afrika kuikabili timu ya Taifa ya Namibia.

  • Tunisia katika michezo mitano [5] iliyopita ameshinda michezo mirltatu [3], imepoteza mchezo mmoja [1] na kutoa sare mchezo mmoja [1].
  • Mara ya mwisho Tunisia kupoteza mchezo ilikuwa dhidi ya Japan walipokubali kichapo cha goli 2-0.
  • Kwenye michezo mitano iliyopita Tunisia imefunga magoli saba [7] na imefungwa magoli mawili [2].
  • Katika michezo mitano [5] iliyopita Namibia imeshinda mchezo mmoja [1], sare tatu [3] na imepoteza mchezo mmoja [1].
  • Mara ya mwisho Namibia kupoteza mchezo ilikuwa dhidi ya Equatorial Guinea walipo chapwa goli 1-0.
  • Namibia katika michezo mitano [5] ya mwisho, imefunga magoli mawili [2] na imeruhusu goli moja [1].
  • Kwa takwimu hizi Namibia imekuwa timu ngumu sana kuruhusu magoli na kufunga pia lakini Tunisia ina ukuta imara na inafunga sana magoli, hii ni moja ya mechi bora sana kuitazama.
  • Tunisia ipo nafasi ya 28 kwa ubora Duniani, na Namibia ipo nafasi ya 115 kwa ubora Duniani.

Popular Posts

Exit mobile version