NBC Premier League

AZAM NI BORA ZAIDI YA SIMBA MSIMU HUU.

Published on

Ligi kuu kandanda Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea hii leo kwa mchezo mmoja kupigwa jijini Mwanza kati ya Simba dhidi ya Azam FC majira ya saa 10:00 Jioni.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa katika uwanja wa CCM Kirumba na kuelekea mchezo huu hizi ndizo takwimu pindi timu hizi zinapokutana.

  • Mechi – 20
  • Simba Ushindi – 7
  • Azam Ushindi – 5
  • Sare – 8

Azam imeshinda michezo yake yote mitano [5] ya mwisho ya Ligi, ipo nafasi ya pili [2] na Simba imeshinda michezo mitatu [3] na sare mbili [2], ipo nafasi ya tatu [3] ya msimamo.

Msimu huu klabu ya Azam FC imepoteza michezo miwili [2] na kutoka sare mchezo mmoja [1], imeshinda michezo kumi [10] katika michezo 13 iliyocheza.

Simba imepoteza mchezo mmoja [1] na sare michezo miwili [2], na imeshinda michezo tisa [9] katika michezo 12 iliyocheza msimu huu.

Simba imefunga magoli 28, imeruhusu magoli 13 na Azam imefunga magoli 35 na kuruhusu magoli kumi [10] msimu huu.

Mechi ya leo itaamua timu ipi ishike nafasi ya pili na kivyovyote vile nafasi ya kwanza haitaguswa na yoyote tofauti na Yanga vinara.

Popular Posts

Exit mobile version