Connect with us

Taifa Stars

TAIFA STARS YAPANDA NAFASI MBILI UBORA DUNIANI.

Tanzania imepanda nafasi mbili juu kwenye viwango vya shirikisho la soka Duniani FIFA kwa mwezi wa pili [February] zilizotolewa hii leo.

Tanzania kabla ya kupanda ilikuwa nafasi ya 121 ikiwa na alama 1155.19 na sasa imepanda hadi nafasi ya 119 ikifikisha alana 1160.98.

Tanzania imeongeza alama 5.79 kutokana na kiwango walichokionyesha kwenye michezo ya fainali za mataifa ya Afrika zilizomalizika hivi karibuni nchini Ivory Coast.

Tanzania inashika nafasi ya 30 Barani Afrika ikiwa imepanda kwa nafasi mbili juu kutoka nafasi ya 32.

Kinara Duniani.

  • Argentina
  • Ufaransa
  • England

Vinara Afrika

  • Morocco
  • Senegal
  • Nigeria

Ukanda wa Cecafa

  • Uganda
  • Kenya
  • Tanzania.

Makala Nyingine

More in Taifa Stars