Kwa mujibu wa taarifa kutoka Italia zinasema klabu ya Chelsea imefikia makubaliano binafsi na mshambuliaji wa klabu ya SSC Napoli raia wa Nigeria Victor Osimhem ili ajiunge na klabu hiyo msimu ujao.
Osimhem yupo tayari na amekubali kujiunga na miamba hiyo ya Jiji la London, kilichosalia kwasasa ni makubaliano baina ya klabu mbili za Chelsea na SSC Napol.