Simba

SIMBA YATEUA BARAZA LA USHAURI.

Simba imewateua wajumbe 24 watakaounda Baraza la ushauri la klabu hiyo.

Published on

Rais wa heshima wa klabu ya Simba Mohammed Dewji kwa kushirikiana na mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu leo wametangaza wamewateua wajumbe wa Baraza la ushauri la klabu ya Simba,kupitia ukurasa wa Instagram Mohammed Dewji amesema kazi yake kama Rais wa heshima ni kuhakikisha uongozi bora.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita tangu tuanze safari ya Mabadililko Klabu yetu imepiga hatua kubwa sana katika nyanja mbali mbali. Pamoja na maendeleo ambayo Klabu yetu imepiga katika kipindi hiki cha miaka mitano lakini malengo yetu bado hatujayafikia.

Mojawapo ya majukumu yangu kama Raisi wa heshima wa Simba ni kuhakikisha Uongozi na Utawala bora unazidi kuboreshwa kila wakati ili kuzidi kusukuma gurudumu la maendeleo ya Klabu yetu.

Mohammed Dewji kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Walioteuliwa kwenye Baraza hilo ni

  1. Jaji Thomas Mihayo M/kiti
  2. Hassan Dalali-Mjumbe
  3. Ismail Aden Rage-Mjumbe
  4. Evans Aveva-Mjumbe
  5. Faroukh Baghoza
  6. Swedi Nkwabi-Mjumbe
  7. Azim Dewji-Mjumbe
  8. Kassim Dewji-Mjumbe
  9. Musleh Al-Ruweh-Mjumbe
  10. Mohamed Nassor-Mjumbe
  11. Mulamu Ng’ambi-Mjumbe
  12. Octavian Mshiu-Mjumbe
  13. Prof Janabi-Mjumbe
  14. Hassan Kipusi-Mjumbe
  15. Geofrey Nyange-Mjumbe
  16. Gerald Yambi-Mjumbe
  17. Moses Kaluwa-Mjumbe
    18.Crescentius Magori-Mjumbe
  18. Juma Pinto- Mjumbe
  19. Mwina Kaduguda-Mjumbe
  20. Idd Kajuna-Mjumbe

Sekretariat ya Simba itaratibu mikutano ya Baraza hili la Ushauri. Kazi kubwa ya Baraza hili itakuwa ni kuishauri Bodi juu ya maendeleo ya Klabu yetu ya Simba, Uongozi na Utawala bora.

Mo Dewji aliongeza.

Popular Posts

Exit mobile version